Majadiliano:Cirta

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Cirta mosaic

Cirta unajulikana kwa majina tofauti ya kale, ilikuwa ni sehemu ya kale iliyokuwa ni makaazi ya Waberber na Waroma na baadaye ulipewa jina la Constantine, Algeria. Cirta ulikuwa ni mji mkuu wa ufalme wa waberber wa Numidia; mji wake muhimu uliopangiwa kimkati kama bandari uliitwa Russicada.Ingawa Numidia ulikuwa na mahusiano muhimu na jamuhuri ya kale ya Roma kipindi cha vita ya punic (264-146),mji Cirta ulikuwa mhanga wa uvamizi kipidi karne ya 1 na 2 kabla ya Kristo.Hatimaye ulikuja kutawaliwa na Warumi wakati wa kaisari Julius.Cirta uliitawaliwa na Warumi katika kipindi cha Kaisari na Agustus na ulizungukwa na maeneo ya "shirikisho la miji huru ya Roma" kama Chullu, Rusicade, na Milevum, uliongozwa mwanzoni na Publius Sittius.Mji uliharibiwa mwanzaoni mwa karne ya 4 na ulijengwa upya na kaisari wa Roma Constantine, ambae aliupa mji huo jina jipya la Constantine.Wavandal waliuharibu mji wa Cirta, lakini kaisari Justinian I akaunyakua na kuurekebisha mji huo wa Waroma.Uliipungua umuhimu wake baada ya uvamizi wa Waislamu, lakini jamii ndogo iliendelea kwa muda wa karne kadhaa.Magofu yake yamefanywa kama makumbusho ya kihistoria.

Marejeo[hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Algeria bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Majadiliano:Cirta kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.