Kisotho-Kaskazini
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kisotho-Kaskazini (pia Kisepedi) ni lugha ya Kibantu hasa nchini Afrika Kusini inayozungumzwa na Wasepedi. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kisotho-Kaskazini nchini Afrika Kusini imehesabiwa kuwa watu zaidi ya milioni nne. Pia kuna wasemaji 11,000 nchini Botswana. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kisotho-Kaskazini kiko katika kundi la S30.
[hariri] Viungo vya nje
| Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kisotho-Kaskazini kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |