Kikami (Tanzania)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta

Kikami ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wakami. Isichanganywe na lugha ya Kikami nchini Nigeria.

Viungo vya nje [hariri]

Marejeo [hariri]

  • Maho, Jouni na Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) Göteborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Uk ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Seidel, Agosti. 1896. Beiträge zur Kenntnis des Ki-Kami in Deutsch-Ostafrika. Zeitschrift für afrikanische und oceanische Sprachen, 2, uk 3–32.
  • Velten, Carl. 1900. Kikami, die Sprache der Wakami in Deutsch-Ostafrika. Mitteilungen des Seminars für orientalische Sprachen, 3 (III. Abt.), uk 1–56.

Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.