Kianyin
Kianyin ni lugha ya Kiniger-Kongo nchini Cote d'Ivoire na Ghana inayozungumzwa na Waanyin. Mwaka wa 1993 idadi ya wasemaji wa Kianyin nchini Cote d'Ivoire imehesabiwa kuwa watu 610,000. Tena mwaka wa 2003 kumehesabiwa wasemaji 250,000 nchini Ghana. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kianyin kiko katika kundi la Kikwa.
Viungo vya nje [hariri]
- lugha ya Kianyin kwenye Multitree
- ramani ya Kianyin
- http://www.ethnologue.org/show_language.asp?code=any
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.