Ikonografia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Theotokos wa Tikhvin, mchoro wa mwaka 1300 hivi.

Ikonografia (kutoka Kigiriki εἰκών, eikon, "picha" na γράφειν, grafein, "kuandika" kupitia Kiingereza "iconography") ni tawi la historia ya sanaa ambalo linachunguza asili na maana ya picha kama sanaa[1][2][3].

Utaalamu huo unahitajika hasa katika kufafanua picha takatifu za Ukristo wa Mashariki, kwa kuwa hizo hazilengi kuiga sura halisi zinavyoonekana na macho, bali kudokeza mafumbo ya imani ili kuona yasiyoonekana.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]