Shirika la Kimataifa la Usanifishaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka ISO)

Shirika la Kimataifa la Usanifishaji (kwa kifupi ISO) ni shirika lenye wajibu wa kuandaa na kutekeleza vipimo vya pamoja kwa sehemu mbalimbali za teknolojia na uchumi duniani. Jina limechaguliwa kutokana na neno la Kigiriki ίσος (isos) linalomaanisha "sawa".

Kuna mashirika mawili yanayoshirikiana nalo ambayo ni Kamati ya Kimataifa kwa Teknolojia ya Umeme na Umoja wa Kimataifa wa Vyombo vya Mawasiliano yanayoshughulika teknolojia za kuhusiana na fani zao na zote kwa pamoja ni Umoja wa Usanifishaji wa Dunia.

ISO iliundwa mwaka 1947 kama ushirikiano wa nchi 25 zilizoamua kuunganisha jitihadi zao za usafinishaji. Makao makuu yako Geneva (Uswisi). Hadi leo kuna nchi wanachama 163 kati ya mataifa 203 za dunia.

Vipimo vinavyokubaliwa hutolewa namba inayoanza kwa herufi ISO kwa mfano ISO 8601 kuhusu namna ya kuandika wakati na tarehe, ISO 4217 kuhusu kutaja hela za nchi za dunia au ISO 668 inayotawala vipimo vya kontena zinazokubaliwa katika biashara ya kimataifa.


Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Tovuti ya ICO (Kiing.) Archived 25 Januari 2007 at the Wayback Machine.