Dele Adebola

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Bamberdele Olusegun Adebola (alizaliwa Lagos, Jimbo la Lagos, 23 Juni 1975) ni mchezaji wa soka wa Nigeria aliyestaafu. Amecheza kwa vilabu 16 katika kazi yake, akiwa amekopwa mara kadhaa, na vipindi vyake virefu zaidi vikiwa ni katika vilabu vya Crewe Alexandra, Birmingham City, na Coventry City.

Maisha ya Awali[hariri | hariri chanzo]

Adebola alikulia huko Liverpool baada ya kuwasili nchini Uingereza akiwa mtoto na familia yake; akiwa kama mwanafunzi, alicheza katika timu za wawakilishi sawa na Robbie Fowler. Alipokewa nafasi ya YTS na Liverpool, timu ambayo alikuwa akiishabikia, aliamini kwamba kujaribu kufanikiwa kama mshambuliaji wa mguu wa kushoto katika klabu wakati huohuo na Fowler haingekuwa wazo nzuri. Kwa hivyo, alikubali nafasi kama hiyo kutoka Crewe Alexandra.[1][2]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Culley, Jon. "Adebola out to upstage an old idol", 24 Februari 2001. 
  2. Szreter, Adam. "Adebola lifts the Blues", 5 Septemba 1998. 
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dele Adebola kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.