Andrey Marcel Ferreira Countinho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Andrey Marcel Ferreira Countinho
Maelezo binafsi
Jina kamili Andrey Marcel Ferreira Countinho
Tarehe ya kuzaliwa 12 Januari 1990 (1990-01-12) (umri 34)
Mahala pa kuzaliwa    Brasilia, Brazil
Urefu m1.70
Nafasi anayochezea Mlengo wa kushoto
Maelezo ya klabu
Klabu ya sasa Kwampong
Namba 7
Klabu za ukubwani
Miaka Klabu
Santa Cruz 2009-2012

Taubate 2012-2014

Yanga Sc 2014-2016

Kwampong 2016-

* Magoli alioshinda

Andrey Marcel Ferreira Countinho (amezaliwa 12 Januari 1990) ni mchezaji wa kandanda kutoka Brazil akiichezea klabu ya Kwampong kutoka Korea Kusini akicheza nafasi ya mrengo wa kushoto, pia ana uwezo wa kucheza nafasi ya kiungo mshambuliaji.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Andrey Countinho ni mmoja ya wachezaji wanaopiga faulo kwa ufundi ikiwa anaichezea Santa Cruz kafunga faulo 6 na Taubate 7 na Yanga kafunga faulo 4 mpaka Julai 2015.

Wasifu wa mapema[hariri | hariri chanzo]

Andrey Countinho alianzia soka katika timu ya Vijana ya Santa Cruz ya nchini Brazil ilikuwa mwaka 2007 alipandishwa timu ya wakubwa mwaka 2009 Countinho alicheza mchezo wake wa kwanza mwaka 2010 february akitokea nje ilikuwa dhidi ya Vasco da Gama Countinho alifunga goli lake la kwanza dhidi ya Menereila da santo ilikuwa mnamo mwezi Aprill katika ushindi wa 2 bila Andrey alianza kucheza katika kiwango kizuri mwaka 2011 na Taubate wakaanza kumnyatia na wakamsajiri

Nafasi Timu ya Taifa[hariri | hariri chanzo]

Andrey Countinho ajawahi kucheza timu ya Taifa ya Brazil kutokana na nafasi finyu iliyopo Taifa hilo ndipo Andrey anataka achukue utaifa wa Tanzania ili aweze kushiriki michuano ya Kimataifa.

Atua nchini Tanzania[hariri | hariri chanzo]

Andrey alisajiliwa nchini Tanzania katika klabu ya Yanga Sc; bao lake la kwanza la ligi lilikuja mnamo Octoba 2014 ulikuwa mchezo dhidi ya Tanzania Plizons Fc akifunga kwa faulo.

Mashindano ya kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Andrey Countinho ameshiriki mashindano matatu Africa ambayo ni Kombe la Mapinduzi African Cup Confederation kombe la Shirikisho na Kagame Cup Cecafa Kombe la mabingwa Africa Mashariki.

Tuzo[hariri | hariri chanzo]

Andrey amenyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi katika Timu yake ya Yanga Sc nchini Tanzania pia alifunga magoli manne katika kombe la Mapinduzi Januari 2015

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Andrey Marcel Ferreira Countinho kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.