Uswisi
Uswisi |
---|
Uswisi ni nchi ya Ulaya isiyo na pwani katika bahari yoyote.
Imepakana na Ujerumani, Ufaransa, Italia, Austria na Liechtenstein.
Jina rasmi ni Confoederatio Helvetica (kwa Kilatini: Shirikisho la Kiswisi).
Majimbo yake 26, ambayo huitwa "kantoni", yanajitawala.
Historia[hariri | hariri chanzo]
Shirikisho la Uswisi lilianza mwaka 1300 hivi kutokana na ushindi vitani dhidi ya Austria na Burgundy.
Uhuru wa shirikisho kutoka Dola Takatifu la Kiroma ulitambuliwa rasmi katika Amani ya Westphalia mwaka 1648.
Sifa[hariri | hariri chanzo]
Uswisi imepata umaarufu hasa kutokana na sababu zifuatazo:
- ni nchi isiyoshiriki katika vita kwa zaidi ya miaka 300
- ni nchi ambapo watu wenye utamaduni tofauti na nchi jirani wameshirikiana karne nyingi kwa amani
- ni nchi iliyotunza demokrasia tangu karne nyingi bila kuwa na vipindi vya udikteta au utawala wa mabavu, tena demokrasia ya moja kwa moja ambako wananchi wa kawaida wana haki ya kutunga au kubadilisha sheria kwa njia ya kura ya maoni ya watu wote
- ni nchi yenye benki zenye sifa kote duniani
Miji[hariri | hariri chanzo]
Mji mkuu wa shirikisho ni Bern.
Mji mkubwa ni Zürich wenye benki nyingi.
Mji wa Geneva ni kati ya makao makuu ya Umoja wa Mataifa; ni pia makao makuu ya kimataifa ya Umoja wa shirika za Msalaba Mwekundu na mashirikia mengine ya kimataifa.
Hata hivyo Uswisi imekuwa kati ya nchi za mwisho kujiunga na UM (2002).
Watu[hariri | hariri chanzo]
Kuna lugha rasmi 4: Kijerumani (62.8%), Kifaransa (22.9%), Kiitalia (8.2%) na Kirumanj (0.5%). Lakini wengi wanajua na kutumia lugha zaidi ya moja.
Kati ya lugha za kigeni zinazotumika nyumbani, zinaongoza Kiingereza (5%), Kireno (3.8%), Kialbania (3%), Kihispania (2.6%), Kiserbokroatia (2.5%) n.k.
Upande wa dini, kati ya wakazi, 68% ni Wakristo, hasa Wakatoliki (37.2%) na Wakalvini (25%), lakini pia Waorthodoksi (2.3%) na wengineo. 5.1% ni Waislamu (hasa wahamiaji). 24% hawana dini maalumu.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- (Kiingereza) (Kifaransa) (Kijerumani) (Kiitalia) Serikali ya Uswisi (Swiss Federal Authorities) Archived 3 Januari 2005 at the Wayback Machine.
- (Kiingereza) The Swiss Confederation: A Brief Guide 2006 Archived 15 Juni 2006 at the Wayback Machine.
- (Kiingereza) Switzerland information at Traveldir.org Archived 10 Agosti 2006 at the Wayback Machine.
- Pictures from Switzerland Archived 8 Septemba 2006 at the Wayback Machine.
Makala hii kuhusu maeneo ya Uswisi bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Uswisi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |