Latvia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Latvijas Republika
Jamhuri ya Latvia
Bendera ya Latvia Nembo ya Latvia
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Tēvzemei un Brīvībai
(Kilatvia: " Kwa taifa na uhuru ")
Wimbo wa taifa: Dievs, svētī Latviju!
(Kilatvia: "Mungu ubariki Latvia!")
Lokeshen ya Latvia
Mji mkuu Riga
56°57′ N 24°6′ E
Mji mkubwa nchini Riga
Lugha rasmi Kilatvia
Serikali Demokrasia
Egils Levits
Arturs Krišjānis Kariņš
Uhuru
Ilitangazwa (kutoka Urusi)
Ilitambuliwa
Ilitangazwa
(mwanzo wa kuachana na
Umoja wa Kisovyeti)

Ilikamilishwa

18 Novemba 1918
26 Januari 1921
4 Mei 1990


6 Septemba 1991
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
64,589 km² (ya 124)
1.5
Idadi ya watu
 - Julai 2014 kadirio
 - 2011 sensa
 - Msongamano wa watu
 
1,973,700 (ya 148)
2,070,371
34.3/km² (166)
Fedha Euro (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
EET (UTC+2)
EEST (UTC+3)
Intaneti TLD .lv 1
Kodi ya simu +371

-


Ramani ya Latvia

Latvia (kwa Kilatvia: Latvija au Latvijas Republika, kwa Kilivonia: Lețmō au Leţmō Vabāmō) ni nchi ya Kibalti katika Ulaya ya Kaskazini.

Imepakana na Estonia, Lithuania, Belarus na Urusi. Uswidi iko ng'ambo ya bahari ya Baltiki.

Mji mkuu ni Riga.

Latvia ni nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 1 Mei 2004.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kwa muda mrefu Estonia ilikuwa chini ya Wajerumani, Wapolandi na Waswidi, halafu (1710) sehemu ya Dola la Urusi.

Katika miaka 1918-1940 ilikuwa jamhuri halafu miaka 1940-1991 mwanachama wa Umoja wa Kisovyeti.

Baada ya umoja huo wa majimbo 15 kusambaratika, Latvia ilijitangaza nchi huru tena.

Latvia ilijiunga na Umoja wa Ulaya baada ya azimio la Halmashauri Kuu ya Ulaya ya tarehe 13 Desemba 2002 iliyokutana Kopenhagen.

Katika kura ya maoni ya tarehe 20 Septemba 2003 ni 66.9% za Walatvia wote waliokubali azimio hilo.

Latvia iliingia rasmi katika Umoja wa Ulaya tarehe 1 Mei 2004 pamoja na nchi nyingine 9 za Ulaya mashariki.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Idadi ya watu inapungua, na sasa iko chini ya milioni 2.

Wakazi wengi ni Walatvia 61.6%, halafu Warusi 25.8%, Wabelarus 3,4%, Waukraina 2,3%, Wapolandi 2,1%, Walituania 1.2% na wengine 4.8%.

Lugha rasmi ni Kilatvia, ambayo ni mojawapo ya lugha za Kibalti. Wananchi walipiga kura ya kukataa Kirusi kama lugha rasmi ya pili.

Upande wa dini, wengi (78.5%) ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, ingawa 7% tu wanashiriki ibada mara kwa mara. Hasa ni Walutheri (34.2%), Wakatoliki (24.1%) na Waorthodoksi (19.4%). Asilimia 21.1 hawana dini yoyote.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Latvia
Nchi za Kibalti
Mengineyo

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Serikali
Taarifa za jumla
Elimu na utamaduni
Utalii
Ramani


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Latvia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.