Studio ya kurekodia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Studio ya Kurekodia)
Mchezaji anapiga tarumpeta katika sehemu ya studio na fundi sauti anarekodi katika chumba cha dhibiti

Studio ya kurekodia ni mahali palipoandaliwa kwa kurekodi sauti hasa muziki. Studio za aina hii hutawaliwa na watu binafsi au mara nyingi na makampuni ya kurekodia yanayouza rekodi kama DVD au CD za muziki. Studio ndogo zinatumiwa pia na wanamuziki wanaotaka kuwa na kumbukumbu ya binafsi au kuuza rekodi zao wenyewe. Hapa watumiaji wanalipa kodi fulani kwa masaa ya matumizi.

Jengo na mitambo[hariri | hariri chanzo]

Studio ya kurekodia inahitaji jengo au vyumba vyenye ujarabati sauti yaani aina za hami zinazozuia sauti na makelele ya nje kufika ndani.

Ndani ya studio kuna sehemu mbili

  • studio yenyewe yaani chumba au vyumba ambako wanamuziki wanaimba au kupiga ala zao.
  • chumba cha dhibiti ambako fundi sauti na wasimamizi wanasikiliza na kurekodi wakimtazama mwanamuziki dirishani na kusikia sauti kupitia mitambo.
  • Studio kubwa huwa pia na chumba cha pekee kwa ajili ya mitambo kwa kuzuia usumbufu kutokana na sauti za vipozaji vya kompyuta n.k.

Fundi sauti anatumia mitambo yake kupokea sauti na kuibadilisha kwa ajili ya rekodi za kuuzwa kwa kusahihisha marudio sauti, mahadhi na kadhalika; pia anaweza kufupisha rekodi au kuunganisha rekodi mbalimbali.