Paulino wa Trier

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake.

Paulino wa Trier (alizaliwa Gascony, Ufaransa[1] - alifariki Frigia, leo nchini Uturuki, 358) alikuwa askofu wa mji huo (leo nchini Ujerumani) kuanzia mwaka 346.

Alitetea imani sahihi dhidi ya Uario, na katika Sinodi ya Arles, iliyoitishwa na kaisari Konstans II ili kumlaani Atanasi wa Aleksandria, alikataa peke yake asijali vitisho wala mabembelezo [2][3].

Kwa ajili hiyo alipelekwa uhamishoni alipofariki baada ya miaka 5 ya mateso[4].

Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 31 Agosti[5][6].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.