Nemesi wa Aleksandria

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nemesi wa Aleksandria (alifariki 250 hivi) alikuwa Mkristo wa Misri aliyefia dini kwa kuchomwa moto katika mji huo wakati wa dhuluma ya kaisari Decius.

Kabla ya hapo aliwahi kufungwa kwa kusingiziwa kuwa mwizi, lakini mahakama ilithibitisha si kweli. Lakini dhuluma hiyo ilipoanza, alikamatwa tena na kushtakiwa mbele ya hakimu Emiliani kwamba ni Mkristo, na kwa amri yake aliteswa tena na tena na hatimaye kuhukumiwa achomwe moto pamoja na wezi, kwa mfano wa Yesu aliyesulubiwa pamoja na wahalifu wawili[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi wa Mashariki, Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 10 Septemba[2] lakini pia 19 Desemba[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.