Leokrisya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Leokrisya alivyochorwa akishuhudia kifodini cha Eulogi wa Cordoba.

Leokrisya (alifariki Cordoba, Hispania, 15 Machi 859) alikuwa binti wa familia ya Kiislamu aliyeacha dini hiyo ajiunge na Kanisa Katoliki.

Alipokamatwa nyumbani pamoja na askofu Eulogi wa Cordoba alikatwa kichwa na Waislamu waliotawala nchi hiyo kwa sababu alikataa katakata kurudi nyuma[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Machi[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

  • Tolan, John, Medieval Christian Perceptions of Islam, New York: Routledge, 2000. ISBN 0-8153-1426-4

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.