Klod

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Klod.

Klod (kwa Kifaransa Cloud; kwa Kilatini Clodoaldus; 522 - 560 hivi) alikuwa padri kutoka ukoo wa kifalme wa Orleans huko Ufaransa [1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Septemba[2].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Babu yake alikuwa Klovis I na bibi yake alikuwa mtakatifu Klotilda malkia.

Baba yake, mfalme Klodomer[3], na ndugu zake wawili waliuawa wakiwa bado watoto; yeye tu alinusurika kwa kumkimbilia bibi yake huko Provence[4] na kujinyima haki zote za kurithi. Pia aliwagawia fukara mali iliyombakia.

Baada ya kuishi kama mkaapweke chini ya Severini wa Paris, alipoona anatembelewa na watu wengi kwa ushauri kiasi kwamba hafaidiki na upweke akarudi Paris, alipopokewa kwa furaha.

Watu walimuomba askofu ampe upadrisho (551). Halafu alitoa huduma kwa muda fulani, kisha akarudi upwekeni, na hatimaye akaanzisha abasia karibu na Versailles[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.