Maghani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Maghani (au mighani kutoka neno la Kiarabu) ni utanzu wa kifasihi simulizi unaoonyesha matukio ya kijasiri na kishujaa ya mtu au watu katika kipindi fulani cha maisha.

Maghani katika Fasihi Simulizi[hariri | hariri chanzo]

Maghani ni tungo zinazotolewa kwa kughanwa (nusu kuimbwa nusu kukaririwa).

Maghani yanaweza kuambatanishwa na ala za muziki au kughanwa kwa mdomo tu.

Aina za Maghani[hariri | hariri chanzo]

Zipo fani mbalimbali za maghani ambazo zimeainishwa katika tanzu mbili kuu: 1. Maghani ya Kawaida 2. Maghani ya Masimulizi

Maghani ya Masimulizi[hariri | hariri chanzo]

Lengo la maghani ya aina hii ni kusimulia kisa fulani, historia, n.k.

Kuna fani mbili za Maghani ya Masimulizi: a) Tendi Tendi ni ushairi mrefu unaosimulia matukio ya kishujuaa. Tendi zinaposimuliwa huandamana na ala za muziki. Sifa za Tendi: • Ni ushairi mrefu • Husimulia matendo ya kishujaa kwa njia kishairi • Husimuliwa badala ya kuimbwa • Huandamana na ala za muziki • Husimulia visa vya kihistoria • Hutungwa papo kwa hapo

b) Rara Hizi ni hadithi fupi za kishairi zenye visa vya kusisimua, zinazosimuliwa zikiambatanishwa na ala za muziki. Aghalabu hughanwa na watoto; na hutumika kama michezo ya watoto. Sifa za Rara • Ni hadithi fupi za kishairi • Husimulia visa vya kusisimua • Zinaweza kuimbwa au kusimuliwa • Huambatana na ala za muziki • Aghalabu huwa ni visa vya kubuni

Maghani ya Kawaida (Sifo)[hariri | hariri chanzo]

Maghani ya Kawaida ni maghani yanayosifia mtu, kitu au hali katika jamii a) Majigambo au Kivugo Haya ni maghani ambayo mtunzi hujisifia (kujigamba) namna alivyo hodari katika nyanja fulani. Tungo hizi hutumia chuku na maneno ya kejeli kuwadunisha wapinzani wa mtunzi. Sifa za Majigambo • Hutumia nafsi ya kwanza • Msimulizi hutumia maneno ya kujigamba • Msimulizi hutumia chuku kwa wingi ili kujisifu • Hutungwa kwa ubunifu mkubwa na hutumia mbinu kama sitiari, vidokezi, ishara n.k • Majigambo mengi huwa mafupi, lakini baadhi yake huwa marefu. • Huwa na matendo matukufu ya msimulizi • Huwa na ahadi za matendo kutoka kwa msimulizi

b) Tondozi Tondozi ni aina ya sifo ambayo husifia watu mashuhuri katika jamii kama vile viongozi Sifa za Tondozi • Huwa ni ushairi wa kusimuliwa • Husifia mtu mwengine, mtu mashuhuri • Hutumia chuku • Hutumia mbinu kama sitiari, vidokezi, ishara n.k • Hutaja matendo makubwa ya kiongozi anayesifiwa

Pembezi[hariri | hariri chanzo]

Pembezi ni maghani ya kumsifu mpenzi. Sifa za Pembezi • Humsifu mpenzi wa mtu • Aghalabu huwa ushairi mfupi • Hutumia tamathali za lugha kwa wingi kama vile ishara kusimulia umbo la mpenzi • Pembezi zinaweza kuandamana na ngoma ii) Pembezi - tungo za sifa. Zinaweza kusifia kundi fulani la watu, wanyama, njaa, mvua, n.k

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Oriedo, Hannington. 2007. Istilahi za Fasihi ya Kiswahili, uk.47.
Makala hii kuhusu mambo ya fasihi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Maghani kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.