Kividunda

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kividunda ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na kabila dogo la Wavidunda, wanaoishi katika wilaya ya Kilosa, mkoa wa Morogoro. Mwaka wa 1987 idadi ya wasemaji wa Kividunda imehesabiwa kuwa watu 32,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kividunda iko katika kundi la G30. Kinafanana hasa na Kiluguru, lakini pia na Kihehe na lugha nyingine za kandokando.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Maho, Jouni & Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) Göteborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Pp ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Beidelman, Thomas. 1966. Notes on the Vidunda of eastern Tanganyika: an ethnographic survey. Tanganyika notes and records, 65, uk.63-80.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kividunda kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.