Leonardo wa Portomaurizio

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Leonardo akiwa amevaa kanzu yake ya Kifransisko.

Leonardo wa Portomaurizio (Porto Maurizio, leo Imperia, 20 Desemba 1676 - Roma 26 Novemba 1751), alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo na padri wa Kanisa Katoliki kutoka Italia.

Ndiye tunda bora la Kirekebisho cha utawa wa Ndugu Wadogo kilichoanzia mjini Roma karne XVII.

Ni maarufu hasa kwa mahubiri yake ya wiki nzima (wiki za uamsho) aliyoyaendesha karibu mfululizo kati ya waamini wa Kanisa Katoliki nchini Italia, akisisitiza hasa ibada kwa mateso ya Yesu kwa kupitia vituo 14 vya njia ya msalaba.

Aliyeendesha wiki hizo mara 343, akiongozana kwa kawaida na mapadri 4 na bradha 1. Baada ya wiki mbili za mahubiri kulikuwa na wiki moja ya maungamo.

Katika miaka 44 aliokoa watu wengi ajabu, na kuinua hali ya roho ya mapadri wanajimbo na watawa katika Italia karibu nzima.

Ndiye mwenezaji mkuu wa Njia ya Msalaba, ibada iliyoanza kustawi katika karne XV ikiwa na vituo 7 hadi 37, mpaka ile ya 14 ilipopewa rehema ya pekee (1686) na hivyo kuenea popote.

Papa Pius VI alimtangaza mwenye heri, halafu Papa Pius IX akamtangaza mtakatifu tarehe 29 Juni 1867.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Sala yake[hariri | hariri chanzo]

Yesu wangu, kwa haki tu na kwa shukrani napaswa kujitoa kabisa kwako, baada ya wewe kujitoa kabisa kwangu...

Wewe umetakasa hisi zangu zote; fanya ziwe zako, zisifurahie tena kilicho kinyume cha sheria yako ya Kimungu.

Umetakasa kumbukumbu yangu; iwe inakukumbuka mfululizo.

Umetakasa utashi wangu; usigeuke kamwe kupenda chochote kuliko wewe.

Basi, kutoka dhati ya moyo wangu nakutolea kama sadaka kamili ya kudumu, kadiri ninavyoweza, mwili wangu na roho yangu, hisi zangu na vipawa vyangu, nilichonacho na jinsi nilivyo.

Ee moto wa Kimungu, choma, Ee Upendo wa Mwenyezi, choma na kuteketeza yale yote yasiyo yako ndani mwangu! Amina.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Summarium processus beatificationis V.S.D. Leon. a P.M. (Rome, 1781)
  • RAFELLO DA ROMA, Vita del P. Leonardo da P.M. (Rome, 1754)
  • JOS. De MASSERANO, Vita del B. Leonardo da P.M. (Rome, 1796), written by the postulator and dedicated to the duke of York, son of James [III] of England
  • SALVATORE DI ORMEA, Vita del B. Leonardo da P.M. (Innsbruck, 1869)
  • L. De CHERANCE, S. Leonard de Port-Maurice (Paris, 1903) in Nouvelle Bibliothèque Franciscaine (1st series), XIII. Chapter xx of this last mentioned work had already appeared in Études Franciscaines, VIII (Paris, 1902), 501-10.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.