Vyombo vya habari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Vyombo vya habari mbalimbali

Vyombo vya habari ni vyombo vya mawasiliano vinavyolenga watu wengi iwezekanavyo kwa shabaha ya kuwapatia habari au burudani.

Mifano yake ni magazeti, redio, televisheni au intaneti.

Asili ya jina la Kiingereza[hariri | hariri chanzo]

Nadharia moja ni kwamba habari ilitengenezwa kwa matumizi maalum ya wingi wa neno mpya katika karne ya 14. Katikati mwa Kiingereza, neno sawa na hilo lilikuwa newes, Nouvelles kwa lugha ya Kifaransa na Neues kwa lugha ya Kijerumani. Kiasi fulani ya endeleo sawa na hilo hupatikana angalau katika lugha tatu za Kislavoni (Kicheki, Kislovakia na Kipolishi), ambapo kunalo neno noviny ( "news"), iliyoendelezwa kutoka neno nový ( "mwezi").

Historia ya kuripoti habari[hariri | hariri chanzo]

Ukusanyaji wa habari ulipoanza, viwango vyake havikuwa vya hali ya juu vikilinganishwa na vya sasa. Ilbidi habari za kuchapishwa kuelezwa kupitia simu hadi kwenye kituo cha habari au kuletwa hapo na mwandishi, ambapo ilipigwa chapa na aidha kupelekwa kutumia huduma ya waya au kuhaririwa na kuwekwa pamoja na habari zingine za aina moja kwa toleo maalum. Leo hii, neno "Mchipuko wa habari" limekuwa muhimu kwani huduma za matangazo na habari za amari (cable news) hutumia teknolojia ya satellite kuleta matukio ya sasa moja kwa moja majumbani mwa watumizi wa huduma hii. Matukio ambayo yalikuwa yanachukua masaa au siku kuwa maarifa ya kawaida katika miji au katika mataifa yanaletwa moja kwa moja kupitia redio, televisheni, simu kiini s, na Internet.

Magazeti[hariri | hariri chanzo]

Miji mengi makubwa yalikuwa na magazeti ya asubuhi na alasiri. Vyombo vya habari viliendelea kuwa na sehemu za kusambaza habari kuogezeka hadi kukaribia kupita kiasi.Hii ilisababisha magazeti za alasiri kufungwa zisipokuwa chache. Magazeti ya asubuhi yanapoteza mzunguko, kulingana na ripoti kutoka majarida wenyewe.

Kwa kawaida, habari zapaswa kuwa na vitu tano vya kawaida (nani, nini, wakati gani, wapi, kwa nini, na pia jinsi gani) katika tukio. Hakuna maswali ambayo yanapaswa kubaki. Magazeti kwa kawaida huandika habari zenye hadithi nzito, kama zile zinazofungamana na uuaji, moto, vita, na kadhalika. Ukitumia mfano wa piramidi uliogeuzwahabari muhimu ndizo zinazoanza. Wasomaji bizi wanaweza kusoma sana au kwa ufupi kulingana na shki yao. Stesheni za mitaa na mitandao yenye miundo lazima zichukua hadithi za habari na kuzivunja katika vipengele muhimu kutokana na vikwazo vya wakati. Chaneli za habari za amari kama Fox News, MSNBC, na CNN zina uwezo wa kuchukua faida ya hadithi, hadithi zenye umuhimu ndogo zikitolewa mhanga, na kutoa habari zinazochipuka kwa kina.

Usawa katika habari[hariri | hariri chanzo]

Mashirika ya habari mara nyingi lengo lao hutarajiwa kuwa usawa; waandishi hudai kwamba wao hujaribu kufukua pande zote za suala bila mapendeleo, ikilinganishwa na watangazaji au wachambuzi, ambao hutoa maoni au dhana ya kibinafsi. Hata hivyo, serikali kadhaa huweka baadhi ya vikwazo au huchunguza mashirika ya habari kama yana mapendeleo. Kwa mfano, nchini Uingereza, mipaka huwekwa na wakala wa serikali, Ofcom (Office of Communications), ambayo ni ofisi ya Mawasiliano. Magazeti na vipindi vya matangazo ya habari nchini Marekani kwa ujumla yanatarajiwa kuepuka mapendeleo isipokuwa makala yaliyodokezwa wazi. Serikali nyingi zenye chama moja zinaendesha mashirika ya habari, ambayo yanaweza kuwasilisha maoni ya serikali.

Hata katika hali ambazo usawa hutarajiwa, ni vigumu kupata usawa, na waandishi wa kibinafsi wa habari wanaweza kuwa na mapendeleo ya kibinafsi, au kuangukia katika shinikizo la kibiashara au kisiasa. Vivyo hivyo, usawa wa mashirika ya habari zinazomilikiwa na mashirika ya conglomerate zaweza kushukiwa katika mwanga wa asili ya motisha kwa vikundi vya habari kuripoti katika njia yenye nia ya kuendeleza maslahi ya kifedha ya conglomerate. Watu binafsi na mashirika ambayo ripoti ya habari imelengwa kwao wanaweza kutumia mbinu za usimamizi wa habari kujaribu kufanya hisia nzuri. Kwa sababu kila mtu ana mtazamo fulani, inatambulika kwamba hakuwezi kuwa na usawa katika kuripoti habari.

Karama ya Habari[hariri | hariri chanzo]

Karama ya habari hufafanuliwa kama maswala kuwa na manufaa ya kutosha kwa umma au hadhira maalumu kuhakikisha umakini wa watazamaji.

Watu wa kawaida si wa karama ya habari hadi wakutane ana kwa ana na hali isiyo ya kawaida au janga. Habari hii hugawanyisha umma katika makundi mawili; wale wachache ambao maisha yao ni ya karama ya habari na umati wa watu ambao huzaliwa, huishi maisha yao na kufa bila vyombo vya habari kuwatambua hata kidogo. Daima habari hupitia maswala ambayo huvutia makini ya watu na hutofautiana na maisha yao ya kawaida. Habari hii hutumiwa kwa uepushaji na kwa hiyo matukio ya kawaida si ya karama ya habari. Hata swala liwe upendo,kuzaliwa, hali ya hewa, au uhalifu, ladha ya waandishi wa habari hukimbilia hali isiyo ya kawaida, ya ajabu.

Swala na karama ya habari ya hadithi inategemea na hadhira, kwani wao huamua ni nini linawafanya wawe au wasiwe na nia. Wakaazi wakizidi, habari ya kuripotiwa ya kimataifa pia yaongezeka, kwani kuna maslahi mapana mbalimbali yanaohusika katika uteuzi wake.

Ni sehemu ya habari tu ambayo huonyesha jumla ya maendeleo duniani.

Kuna wataalamu wanaojumlisha pia vitabu katika historia ya vyombo ya habari tangu kupatikana kwa uchapishaji vitabu; wengine wanaona pia aina za maigizo ya tamthiliya kama vyombo vya habari katika jamii za kale.

Kwa jumla maelezo ya kitaalamu ya vyombo vya habari ilikuwa hadi juzi:

"Mawasiliano kwa vyombo vya habari ni mawasiliano ambako habari zinasambazwa wazi (bila kuzuia au kutenga sehemu ya watu kwa kusudi) kwa njia ya mbinu za teknolojia lakini si moja kwa moja (yaani kupitia umbali) na kutoka upande mmoja (watoa habari na wapokeaji hawabadilishani nafasi zao) kwa wapokeaji waliosambazwa." [1]

Iko wazi ya kwamba tamthiliya haikubaliki na maelezo haya. Lakini tangu kupatikana kwa intaneti hasa Web 2.0 tofauti kati ya watoa habari na wapokeaji imeshaanza kuondolewa kwa mfano kwa njia ya blogu na mitandao ya kijamii.

Vyombo vya habari vya kwanza kwa maana iliyoelezwa juu vilikuwa magazeti. Yalifuatwa na redio na baadaye televisheni. Katika miaka ya kwanza ya sinema filamu fupi za habari zilizoonyeshwa kabla ya filamu kuu zilikuwa pia chombo muhimu cha habari kwa umma.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Gerhard Maletzke: Psychologie der Massenkommunikation. In: Ders.: Kommunikationswissenschaft im "Uberblick. Opladen usw. 1998; 45 f.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Stephens, Mitchell. "The History of News - 3 Ed" Oxford University Press, New York, 2007.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vyombo vya habari kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.