Botswana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Botswana
Lefatshe la Botswana (Kitswana)
Kaulimbiu ya taifa: Pula
"Mvua"
Wimbo wa taifa: Fatshe leno la rona
"Barikiwe ardhi hiyo takatifu"
Mahali pa Botswana
Mahali pa Botswana
Ramani ya Botswana
Ramani ya Botswana


Botswana (yaani: Utswana) ni nchi huru iliyoko Kusini mwa Afrika. Jina rasmi ni Jamhuri ya Botswana.

Mji mkuu wa Botswana ni Gaborone.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

w:North-West District (Botswana)w:Chobe Districtw:Central District (Botswana)w:North-East District (Botswana)w:Ghanzi Districtw:Kweneng Districtw:Kgatleng Districtw:Kgalagadi Districtw:Southern District (Botswana)w:South-East District (Botswana)
Mikoa ya Botswana.

Botswana haina pwani kwenye bahari yoyote. Imepakana na Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Namibia. Mpaka baina ya taifa la Botswana na Zambia ni meta 700 tu na ndio mfupi kuliko mipaka yote ulimwenguni.

Kuna pia feri ya moja kwa moja kati ya Botswana na Zambia kuvukia mto Zambezi.

Jangwa la Kalahari linafunika theluthi mbili za eneo la Botswana.

Moja ya maeneo muhimu nchini Botswana ni delta ya mto Okavango. Ndiyo delta kubwa kabisa duniani, maana yake mdomo wa mto si baharini bali kwenye nchi kavu, maji yakiishia jangwani.

Hifadhi ya taifa ya Chobe.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji-wakusanyaji wa jamii ya Wasani.

Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.

Siasa[hariri | hariri chanzo]

Botswana imekuwa na mfumo wa demokrasia kwa miaka mingi, ikiwa na viongozi ambao huchaguliwa kwa kura ya wananchi wote.

Rais wa jamhuri ni Mokgweetsi Masisi.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Msichana akikusanya chakula katika Delta ya Okavango.

Watu wa Botswana hujiita Batswana kutokana na jina la kabila kubwa kabisa nchini (79%). Kuna wakazi takriban milioni 2.3. Kwa sababu nchi ni kubwa msongamano wa watu kwa kilometa za mraba ni 3.7 pekee. Idadi hiyo ndogo imetokana na sehemu kubwa ya nchi hiyo kuwa jangwa.

Lugha inayotumiwa na wakazi walio wengi ni Setswana (Kitswana) pamoja na Kiingereza.

Upande wa dini, wakazi wengi (73%) ni Wakristo, wakiwemo Waprotestanti (66%) na Wakatoliki (7%). Wafuasi wa dini asilia ya Kiafrika ni 6%. Asilimia 20 haina dini yoyote.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Uchumi wa Botswana umekuwa imara kwa miaka mingi na hali ya maisha imeendelea kuwa bora kila mwaka tangu uhuru.

Utajiri wa nchi unatokana hasa na migodi ya almasi, pamoja na machimbo ya shaba na minerali kama vile chumvi.

Watalii wanaongeza pato la taifa hasa kwa sababu ya uzuri wa delta ya Okavango.

Fedha ya Botswana huitwa Pula (yaani mvua). Ina thebe (="ngao") 100.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Botswana kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.