Lucy Komba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Lucy Komba
Lucy akiwa katika pozi.
Lucy akiwa katika pozi.
Jina la kuzaliwa Lucy Francis Komba
Alizaliwa 24 Oktoba 1980
Jina lingine Roda
Kazi yake Mwigizaji
Mtayarishaji
Mwongozaji
Miaka ya kazi 2002- hadi leo

Lucy Francis Komba (amezaliwa tar. 24 Oktoba 1980) ni mwigizaji wa filamu, mwongozaji na mtayarishaji kutoka nchini Tanzania. Huenda akawa anafahamika zaidi kwa kutayarisha filamu ya Yolanda 1-2 na Utata. Lucy pia ni mmoja kati ya waliokuwa waigizaji wa kundi la sanaa la Kaole Sanaa Group.

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Lucy Francis Komba alizaliwa mnamo tarehe 24 Oktoba ya mwaka wa 1980, katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Alipata elimu yake ya awali (chekechea) katika shule ya St. Peters Nusery School na msingi alisoma katika shule ya Oysterbay Primary School. Elimu ya sekondari alisoma Moshi katika mkoa wa Kilimanjaro, kwa kidato cha 1 - 4 na 5 - 6 alisoma katika shule ya Kibosho Secondary School.

Kwa elimu ya vyuo, alisoma katika Chuo cha Utumishi wa Serikali na alisomea maswala ya IT (Information Technology) na alipata Diploma katika elimu hiyo.

Sanaa[hariri | hariri chanzo]

Sanaa ya awali[hariri | hariri chanzo]

Lucy Komba alianza maswala ya sanaa katika kundi la sanaa la Fukuto Arts Professional. Akiwa huko alishiriki katika baadhi ya mifululizo ya vipindi vya televisheni kama vile "Valentine Day" na "Rangi ya Chungwa".

Baada ya hapo akaelekea zake katika kikundi cha Dar Talent, akiwa huko alipata kushiriki katika filamu moja ya vichekesho. Baada ya hapo alielekea zake katika kikundi cha sanaa cha Kaole Sanaa Group, akiwa huko alipata kushiriki katika mifululizo minne ya vipindi vya televisheni (tamthilia).

Kazi binafsi[hariri | hariri chanzo]

Baada ya kushiriki katika shughuli mbalimbali za uigizaji, Lucy akaamua kufanya kazi zake mwenyewe, yaani kutayarisha, kutunga, kuongoza inakuwa chini yake.

Akiwa anamiliki kazi zake mwenyewe, Lucy alianza kutayarisha filamu ya kwanza kabisa ni ile ya "Utata na ya pili ni "Yolanda" sehemu ya kwanza na ya pili, Vice Versa na Ama Zako Ama Zangu. Mbali na kucheza filamu zake, Lucy pia ameshiriki katika baadhi ya filamu nyingi tu za Tanzania.

Filamu[hariri | hariri chanzo]

Kama mwigizaji[hariri | hariri chanzo]

Lucy Komba.

Kama mtayarishaji/mtunzi/mwigizaji[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: