Zimbabwe
| |||||
Kaulimbiu ya Taifa Unity, Freedom, Work (Kiingereza: Umoja, Uhuru, Kazi) " | | |||||
Wimbo wa Taifa | |||||
Location of Zimbabwe | |||||
Lugha rasmi | Kiingereza na 15 nyingine | ||||
Mji Mkuu | Harare | ||||
Mji mkubwa | Harare | ||||
Rais | Robert Mugabe | ||||
Eneo - Jumla -Maji -Eneo kadiriwa |
km² 390,757 1% ya 60 duniani | ||||
Umma - Kadiriwa - Sensa, - Msongamano wa watu |
13,061,239 ya 66 duniani (2012) ; 32/km² ; ya duniani | ||||
Chumo cha uchumi - Jumla - kwa kipimo cha umma |
$24.99 billion (Orotha ya nchi GDP (kidogo)) $2,100 (Orodha ya nchi kulingana na GDP kwa umma) | ||||
Uhuru - Kadirifu - Barabara |
(kama Rhodesia) 11 Novemba 1965 (kama Zimbabwe) 18 Aprili 1980 | ||||
Fedha | Dolar ya Marekani| | ||||
Saa za Eneo | UTC +2 | ||||
Intaneti TLD | .zw | ||||
kodi za simu | 263 |
Jamhuri ya Zimbabwe (iliyojulikana wakati wa ukoloni kama Rhodesia ya Kusini) ni nchi isiyo na bahari iliyoko upande wa kusini wa Bara la Afrika, kati ya mto Zambezi na mto Limpopo.
Imepakana na Afrika ya Kusini upande wa kusini, Botswana upande wa magharibi, Zambia upande wa kaskazini-mashariki, na Msumbiji upande wa mashariki.
Jina
Jina Zimbabwe linatoka katika jina "dzimba dzamabwe" kumaanisha "nyumba ya mawe" kwa lugha ya Kishona. Nyumba hiyo ya mawe , ambayo imehifadhiwa kama eneo la kihistoria, ilikuwa Milki ya Mwenemtaba ambaye ufalme wake uliongoza eneo hilo miaka ya kale.
Eneo
Zimbabwe imegawiwa katika mikoa 8 na miji miwili ikiwa na hadhi ya Mikoa. Imegawiwa zaidi katika wilaya 59 na manispaa 1,200.
- Bulawayo (mji),
- Harare (mji),
- Manicaland,
- Mashonaland ya kati,
- Mashonaland Mashariki,
- Mashonaland Magharibi,
- Masvingo,
- Matabeleland Kaskazini,
- Matabeleland Kusini na
Miji minne mikubwa ya Zimbabwe ni:
Tazama pia
Historia
Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.
Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.
Tangu karne ya 11, Zimbabwe ya leo imekuwa na falme imara kwenye njia muhimu ya biashara.
Kampuni ya British South Africa ya Cecil Rhodes iliweka mipaka ya sasa katika miaka ya 1890.
Koloni la Uingereza lilianzishwa mwaka 1923 kwa jina la Southern Rhodesia.
Mwaka 1965, serikali ya walowezi Wazungu ilijitangazia uhuru kwa jina la Rhodesia tu.
Baada ya miaka 14 ya kutengwa kimataifa na kupigana na raia Waafrika katika miaka ya 1970, mapatano ya mwaka 1979 yalikubali wakazi wote wawe na haki ya kupiga kura na nchi ikawa huru kweli kwa jina la Zimbabwe mwaka 1980.
Rais Robert Mugabe alipata umaarufu katika siasa kama mpiganaji dhidi ya ukoloni lakini pia kama aina ya dikteta aliyerudisha nyuma uchumi wa nchi.
Watu
Wakazi wengi (82%) ni wa kabila la Washona, 14% ni Wandebele, 2% ni wa makabila mengine ya Kiafrika, 1% ni machotara, Wahindi, Wazungu n.k.
Kwa sasa lugha rasmi ni 16. Lugha kubwa ni Kishona (70%) na Kindebele (20%). Kiingereza ni lugha ya kwanza ya asilimia 2.5% za wakazi.
Upande wa dini, 80% ni Wakristo (hasa Waanglikana, Wakatoliki 17%, Wasabato na Wamethodisti). Waliobaki ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika (11%), hawana dini (7%) na Waislamu (1%).
Utamaduni
Makala ya ndani zaidi: Utamaduni wa Zimbabwe
Mawasiliano
Makala ya ndani zaidi: Mawasiliano Zimbabwe Mawasiliano ya simu, mitambo yake yanaendeshwa na Tel-One0, kampuni ya serikali.
Kuna kampuni 3 za (simu za mkononi): Econet Wireless, Net*One na Telecel.
Uhuru
- The Interpreter kiswa(mfasiri), filamu ya mwaka 2005 ambayo yaonyesha kiongozi chuku wa nchi za Afrika, ambaye ya muadhiri Robert Mugabe, akitafuta kuepuka mahakama ya kimataifa ilioamrishwa na baraza ya kimataifa ya kuhifadhi amani ili kumhukumu kwa hatia dhidi ya haki za kibinadamu.
Katika orodha ya uhuru kwa waandishi wa habari mwaka 2004 Zimbabwe ilishika nafasi ya 155 kati ya nchi 167.
Tanbihi
Viungo via nje
Serikali
- [1] Tovuti rasmi ya Bunge la Zimbabwe
- [2] Tovuti rasmi ya serikalimirror site
Habari
- Ardhi na siasa-BBC usanifu wa utekelezaji wa arthi.
- [3] Zimbabwe destruction: (hadithi ya mtu mmoja)
- New Zimbabwe UK-Based independent daily newspaper
- AllAfrica.com - Zimbabwe news headline links
- IFEX - Zimbabwe press freedom violations
- The Sunday Mirror weekly newspaper
- Zimbabwe Independent weekly newspaper
- The Zimbabwean UK-based independent weekly newspaper (gazeti ya wiingereza)
- The Herald State-owned daily newspaper
- Zimbabwe Situation A comprehensive collection of news stories concerning Zimbabwe from different sources
- Haikona! Zimbabwe News Blog Taarifa ya habari Zimbabwe
Wanamgambo
Mielekezo
- (Chuo kikuu cha kolombia - Zimbabwe maelekezo ya WWW-VL
- Open Directory Project - Zimbabwe maelekezo
- Stanford University - Afrika kusini mwa Sahara: Zimbabwe maelekezo
- Yahoo! - Zimbabwe maelekezo
Utalii
Nyingine
- Amnesty International (Zimbabwe)
- Dariro (makala ya kutafuta vifungu vya Zimbabwe)
- itsbho.com Leading Zimbabwean entertainment website
- RSF report on Zimbabwe from 2003
- Writers of Zimbabwe – (makala ya muadishi kwa waadishi wa Zimbabwe)
- Zimbabwe Human Rights NGO Forum-(haki za kibinadamu)
- ZIMBABWE (viungo via taarifa)
- "Dead Capital" in Zimbabwe
- 5 year archive of Zimbabwe news updated daily
- Zimbabwe Crisis Habari za kuazua zilizo chapishwa wakati wa kura mnamo 2000.
- ZimFest Miziki ya Zimbabwe kila mwaka, Marekani kaskazini.
- Zimbabweb lango la taarifa Zimbabwe
- zwnews Lango la habari Zimbabwe
- Economic Development Bulletin (Maelezo ya maedeleo ya uchumi) kupoteza haki ya mali Zimbabwe na udhoofu wa uchumi.
- Cato Journal Kifungu cha kuanguka kwa nchi ya Zimbabwe
- Center for Global Development (senta ya maedeleo ya dunia) garama na mwanzo wa misukosuko Zimbabwe.
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira |
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Zimbabwe kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |