Yury Luzhkov
Yury Mikhailovich Luzhkov (21 Septemba 1936 – 10 Desemba 2019) alikuwa mwanasiasa wa Urusi alihudumu kama Meya wa Moscow kuanzia mwaka 1992 hadi 2010. Kabla ya kuchaguliwa kwa Gavriil Popov kama meya wa kwanza wa Moscow, yeye pia aliongoza mji huo mkuu katika miaka ya 1990–1991 kama mwenyekiti wa Mosgorispolkom. Alikuwa makamu wa mwenyekiti na mmoja wa waasisi wa chama tawala cha Urusi ya Pamoja (United Russia).
Wakati wa uongozi wa Luzhkov, uchumi wa Moscow ulipanuka na alisimamia miradi mikubwa ya ujenzi jijini humo, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa eneo jipya la kifedha (financial district). Wakati huo huo, alituhumiwa kwa ufisadi, kubomoa majengo ya kihistoria, usimamizi mbovu wa foleni za magari, pamoja na mgogoro wa moshi mzito wa uchafuzi wa mazingira (smog crisis) wakati wa Moto wa nyikani wa Urusi wa 2010. Mnamo tarehe 28 Septemba 2010, Luzhkov alifutwa kazi na aliyekuwa Rais Dmitry Medvedev kupitia those agizo la rais.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Указ о досрочном прекращении полномочий мэра Москвы Archived 8 Oktoba 2010 at the Wayback Machine
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Yury Luzhkov kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |