Wilaya ya Masisi
Mandhari
Wilaya ya Masisi ni wilaya mojawapo ya Mkoa wa Kivu Kaskazini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Eneo la Masisi lina ukubwa wa km2 4,734 na imegawanywa kiutawala katika sekta nne: Bahunde, Bashali, Katoyi, na Osso.[1]
Masisi imepakana na Wilaya ya Walikale upande wa magharibi na kaskazini, Wilaya ya Rutshuru upande wa kaskazini mashariki, Wilaya ya Nyiragongo na Goma upande wa mashariki, na Mkoa wa Kivu Kusini upande wa kusini.
Makao makuu yako katika mji wa Masisi. [1]
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu maeneo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Masisi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |