Wilaya ya Ludewa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Ludewa (kijani) katika mkoa wa Iringa kabla ya umegaji wa mkoa huo.

Wilaya ya Ludewa ni wilaya mojawapo kati ya 6 za Mkoa wa Njombe.

Ludewa iko upande wa kaskazini-mashariki ya Ziwa Nyassa. Wilaya imepakana na wilaya za Njombe na Makete, upande wa mashariki na mkoa wa Ruvuma na upande wa kusini na nchi ya Malawi ng'ambo ya ziwa.

Makao makuu ni mji wa Ludewa.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 151,361 [1]. Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 128,520 [2].

Wenyeji asilia wa Ludewa ni Wapangwa, Wakisi na Wamanda.

Karibu na Lugarawa akiba kubwa ya mtapo wa chuma imetambuliwa kuna mpango wa kuanzisha migodi ya Liganga. Akiba ya madini za chuma ni zaidi ya tani bilioni 1 na hivyo akiba kubwa inayojulikana Afrika. Kuna mradi wa kampuni ya Kichina Sichuan Hongda Group Ltd inayotaka kuzalisha feleji kwa kutumia makaa kutoka akiba ya Mchuchuma karibu na Ziwa Nyasa[3]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz
  2. Sensa ya 2012, Njombe Region
  3. [read:https://www.thecitizen.co.tz/news/Liganga--Mchuchuma-iron-ore--coal-deals-for-review/1840340-5416296-psmqlbz/index.html Liganga, Mchuchuma iron ore, coal deals for review], tovuti ya Citizen TZ, tar. 13.01.2020
Kata za Wilaya ya Ludewa - Mkoa wa Njombe - Tanzania

Ibumi | Iwela | Kilondo | Lifuma | Luana | Lubonde | Ludende | Ludewa | Lugarawa | Luilo | Lumbila | Lupanga | Lupingu | Madilu | Madope | Makonde | Manda | Masasi | Mavanga | Mawengi | Milo | Mkongobaki | Mlangali | Mundindi | Nkomang'ombe | Ruhuhu


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Njombe bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Ludewa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.