Wikipedia:2021 Told Cities Tanzania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Told Cities Tanzania 2021 ni mradi unaolenga kuandika, kuhariri, kuboresha na kuongeza maudhui kuhusu miji mikongwe nchini Tanzania ambayo kiujumla inatambulika na shirika la UNESCO kuwa ni urithi wa Dunia ikiwa ni pamoja na majengo yake. Mradi huu pia unahusisha kuhariri na kuongeza maelezo kwa Kiswahili katika mradi wa Wikidata kuhusu mada hiyohiyo ya miji, majengo ya zamani nchini Tanzania pamoja na majumba ya makumbusho.

Mradi huu unafanyika Tanzania kwa kushirikiana na Kundi la wahariri wa Wikipedia hapa Tanzania na lile la Wiki World Heritage User Group ambao ni kundi la watumiaji wanaojikita katika kuingiza habari za Orodha ya Urithi wa Dunia ya UNESCO katika miradi ya Wikimedia.

Nchini Tanzania majengo ya kale yanayotambulika na UNESCO yanapatikana katika mji mkongwe wa Zanzibar (Zanzibar Stone Town) na pia Kilwa Kisiwani.

Shughuli za mradi huu[hariri chanzo]

Washiriki wa mradi huu wanatakiwa kufanya kazi kuu za aina mbili:

  1. Moja ni kuhariri/kutafsiri makala kutoka Kiingereza kuja Kiswahili, kuboresha makala zilizopo kwa kuongeza picha, na kuhariri maelezo katika Wikidata.
  2. Pili ni wapiga picha kupakia picha mbalimbali za maeneo yoyote nchini Tanzania; picha hizo zinatakiwa kulenga majengo au majumba ya sanaa ya kihistoria ambayo kwa namna fulani huchukuliwa kama ni urithi wa nchi au Dunia kwa ujumla.

Orodha ya makala za kuzifanyia kazi[hariri chanzo]

Mradi huu unalenga kuongeza makala katika Wikipedia hii ya Kiswahili kuhusu maeneo/majengo mbalimbali ya kihistoria yanayotambuliwa katika orodha ya UNESCO. Tovuti ya UNESCO (angalia hapa) inataja majengo 10 za Mji Mkonge lakini inatambua Mji Mkongwe kwa jumla ukiwa pamoja na majengo mengine ya kihistoria.

Sheria ya Zanzibar imeorodhesha majengo 26 kama majengo ya kihistoria ya daraja la kwanza (Town and Country Planning Decree ya 1994; orodha iko uk. 10, Table 4: Grade I listed buildings in the Stone Town), nayo yanaorodheshwa hapo chini. Ramani ya Mji Mkonge inayoonyesha majengo hayo iko hapa.

Katika hatua ya kwanza inawezekana kutafsiri makala kutoka orodha ya Wikipedia ya Kiingereza en:List_of_landmarks_in_Stone_Town, ukiangalia makala zinazohusu majengo yanayotajwa na UNESCO au Sheria ya Zanzibar.

Orodha ya majengo yanayotazamiwa kufanyiwa kazi katika mradi wa Told Cities in Tanzania 2021 (kufuatana na Town and Country Planning Decree ya 1994)
Jina la Kiingereza Jina la Kiswahili Namba (Msimbo) ya Wikidata
Kilosa House Nyumba ya Kilosa, Zanzibar
Former British Consulate Ubalozi Mdogo wa Uingereza, Zanzibar
Mambo Msiige House Nyumba ya Mambo Msiige
Tippu Tip House Nyumba ya Tippu Tip, Zanzibar
Tembo House Nyumba ya Tembo, Zanzibar
Beit al-Ajaib Jumba la Maajabu
Old Fort Ngome Kongwe, Zanzibar
People's Palace Jumba la Sultani, Zanzibar
Royal Tombs Makaburi ya Masultani, Zanzibar
Aga Khan Mosgue Aga Khan Jamaat Khana, Zanzibar
Royal Baths Bafu za Kisultani, Zanzibar
Hindu Temple Hekalu la Kihindu, Zanzibar
StJoseph's Cathedral Kanisa kuu la Mtakatifu Yosefu, Zanzibar
High Court Mahakama Kuu, Zanzibar
State House Ikulu ya Zanzibar
Mnazi Mmoja Hospital Hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar
Peace Memorial Makumbusho ya Amani, Zanzibar
Hamamni Baths Bafu za Hamami, Zanzibar
Minaret of the Shia Ithnasheri Mosgue Mnara wa Msikiti wa Shia Ithnasheri, Zanzibar
Anglican Cathedral Kanisa la Kristo, Zanzibar
Market Building Soko la Darajani, Zanzibar
Darajani Chawl Darajani Chawl, Zanzibar
Khoja Ismaili Charitable Musafarkhana Khoja Ismaili Musafarkhana, Zanzibar
OId Dispensary Zahanati Kongwe, Zanzibar
Bharmal Building Jengo la Bharmal, Zanzibar
Malindi Mnara Mosgue Msikiti wa Malindi, Zanzibar
Sehemu za ziada katika Mji Mkongwe
Jina la Kiingereza Jina la Kiswahili Namba (Msimbo) ya Wikidata
en:Forodhani Gardens Bustani za Forodhani, Zanzibar
NN SS

Kwa Zanzibar tutumie jamii (categories) hizi: [[Jamii:Urithi wa Dunia katika Zanzibar]] [[Jamii:Wilaya ya Mjini Unguja]]; kama ni jumba la makumbusho, tutumie pia: [[Jamii:Makumbusho ya Tanzania]]

Sehemu nyingine ni maghofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara (Ruins of Kilwa Kisiwani and Ruins of Songo Mnara); (ukurasa wa UNESCO hapa). Makala ya enwiki en:Kilwa_Kisiwani ina maelezo mafupi kuhusu majengo kadhaa pamoja na kuonyesha vyanzo vinavyoweza kusaidia kutunga makala, lakini wachangiaji watahitaji kufanya utafiti wa undani zaidi.

Tuzo kwa Washiriki[hariri chanzo]

Mradi huu utatoa tuzo kwa washiriki hai kama ifuatavyo:

  • 150USD, 100USD, na 50USD kwa wahariri bora watatu wa kwanza na
  • 150USD, 100USD, na 50USD kwa wapigapicha bora watatu wa kwanza.