Watakatifu Tisa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Watakatifu Tisa, Axum, Ethiopia.

Watakatifu Tisa walikuwa wamisionari waliochangia sana ustawi wa Ukristo katika Ethiopia ya leo mwishoni mwa karne ya 5. Majina yao ni: Abba Aftse, Abba Alef, Abba Aragawi, Abba Garima (Isaka), Abba Guba, Abba Liqanos, Abba Panteleoni, Abba Sehma na Abba Yemata.

Ingawa wanasemekana kutokea Syria, ukweli ni kwamba wawili au watatu tu walitokea huko; wengine walitokea Konstantinopoli, Anatolia, na hata Roma.[1] Mwanahistoria Tadesse Tamrat anasema walikimbilia Ethiopia ili kukwepa dhuluma zilizofuata Mtaguso wa Kalsedonia.

Kabla yao Ukristo ulikuwa umeishia katika sehemu nyembamba kati ya Adulis na Aksum kwenye njia za misafara[2]

Pamoja na kuongoa wananchi, walianzisha pia idadi ya monasteri zilizopewa kanuni ya Pakomi: Abba Aftse alianzisha ile ya Yeha; Abba Alef ile ya Bi'isa karibu na Mto Mareb; Abba Aragawi ile muhimu ya Debre Damo; Abba Likano na Panteleoni ile ya Axum; Abba Garima nyingine kaskazini kwa Adwa[3][4]; Abba Guba ile ya Madara; Abba Sehma ile ya Sedenya; na Abba Yem’ata ile ya Gar'alta.[5]

Wanasemekana kuwa ndio watafsiri wa Agano Jipya kwenda lugha ya Ge'ez.[6]

Tangu kale wanaheshimiwa kama watakatifu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Paul B. Henze, Layers of Time: A History of Ethiopia (New York: Palgrave, 2000) p. 38.
  2. Taddesse Tamrat, Church and State in Ethiopia, 1270-1527 (Oxford: Clarendon Press, 1972 ISBN 0-19-821671-8), p. 23.
  3. Recent radiocarbon dating supports the tradition of Saint Abba Garima's arrival at the Abba Garima Monastery in 494. The Garima Gospels, which Garima is said to have written, is now regarded as "the world's earliest illustrated Christian manuscript" and the oldest surviving Ethiopian manuscript of any kind.
  4. Martin Bailey. Discovery of earliest illuminated manuscript. ? (June 2010). Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-05-01.
  5. This list is from Richard Pankhurst, The Ethiopians, A history (Oxford: Blackwell, 2001), p.37 n. 38
  6. Shinn, David H.; Ofcansky Bowen, Thomas P. (2013). Historical Dictionary of Ethiopia. United Kingdom: Scarecrow Press Inc. p. 118. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.