Wakonventuali
Utawa wa Ndugu Wadogo Wakonventuali (kwa Kiingereza Order of Friars Minor Conventual, kifupi: OFM Conv, au Wafransisko Wakonventuali) ni tawi la shirika la wanaume lililoanzishwa na Fransisko wa Asizi mwaka 1209.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Wakati wa maisha ya mwanzilishi huyo, baadhi ya Ndugu Wadogo walianza kuishi mijini katika konventi kubwa.
Jambo hilo lilipingwa na wenzao waliopendelea makao ya upwekeni na udogo katika majengo pia.
Ndiyo mwanzo wa farakano kati yao lililokamilika mwaka 1517, ambapo Papa aliwapa ushindi ndugu wa Observansya, yaani waliotaka kushika kikamilifu kanuni ya shirika.
Watakatifu wa tawi hilo ni mapadri Yosefu wa Kopertino na Fransisko Antonio Fasani kutoka Italia Kusini na Maximilian Maria Kolbe kutoka Polandi.
Siku hizi idadi yao ni 4,500 hivi duniani kote.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Ordo Fratrum Minorum Conventualium - Conventual Franciscans Ilihifadhiwa 9 Mei 2008 kwenye Wayback Machine.
- Conventual Franciscan Friars in the United States
- Order of Friars Minor Conventuals Article from the Catholic Encyclopedia
- Friars Minor Conventual in Uganda Greyfriars in Uganda
- VIDEO: OFM Conv - Ordo Fratrum Minorum Conventualium OFM Conv - Ordo Fratrum Minorum Conventualium
![]() |
Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Wakonventuali kama historia yake au maelezo zaidi? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |