Vikta Mwafrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mozaiki katika kanisa lake mjini Milano.

Vikta Mwafrika (kwa Kilatini: Victor Maurus) alikuwa askari Mkristo kutoka Mauretania (katika Algeria ya leo).

Mwaka 303 BK, akiwa Milano (nchini Italia), alibomoa altare kadhaa za dini za jadi za Dola la Roma.

Kwa sababu hiyo aliteswa mbele ya Kaizari Maximian na hatimaye kuuawa pamoja na Waberberi wenzake Nabore na Feliche tarehe 12 Julai huko Lodi (Lombardia)[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na wengineo kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Mei[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/62000
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.