Nenda kwa yaliyomo

Vijili wa Salzburg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Vijili katika kanisa kuu la Salzburg.

Vijili wa Salzburg (kwa Kilatini Vergilius, Virgilius, kwa Kieire Feirgil, Fearghal, 700 hivi - 27 Novemba 784) alikuwa mmonaki mwenye elimu kubwa na mwanaastronomia kutoka Eire.

Mnamo mwaka 743 alihamia Ufaransa, ambapo alipokewa vizuri na mfalme Pipino Mfupi.

Kwa msaada wake, baada ya kuishi miaka miwili huko Cressy, karibu na Compiègne, alikwenda Bavaria, kwa mwaliko wa mtemi Odiloni wa Bavaria, aliyemfanya askofu wa Salzburg (leo nchini Austria) mwaka 748.

Huko alijenga kanisa kuu kwa heshima ya mtangulizi wake Rupati, akajitahidi sana kueneza Ukristo kati ya wananchi wa Karinthia [1].

Alitangazwa mtakatifu na papa Gregori IX mwaka 1233.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake [2].

Mafundisho yake kuhusu umbo la Dunia

[hariri | hariri chanzo]

Vijili alifundisha Dunia kuwa na umbo la tufe na uwezekano wa kuwepo kwa watu upande wa pili wa Dunia.

Kwa sababu hiyo alishtakiwa mbele ya Papa wa Roma kuwa fundisho lake halikulingana na maandiko matakatifu.

Hata hivyo aliweza kujitetea kwa kudokeza kuwa kama upande wa pili wa Dunia kuna watu, wao pia ni watoto wa Adamu walioathiriwa na dhambi yake na ukombozi wa Yesu kama watu wote upande uliojulikana.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  • M. Tangl, Die Briefe des heiligen Bonifatius und Lullus, Berlin, 1916
  • H. Lõwe, Ein literarischer Widersacher des bonifatius. Virgil von Salzburg und die Kosmographie des Aethicus Hister, in «Abhandlungen der geistes- und sozialwissenschaftlichen Klasse, Akademie der Wissenschaften und der Literatur», Mainz, 11, 1951
  • M. L. W. Laistner, Thought and Letters in Western Europe: A.D. 500 to 900, Ithaca, 1955 ISBN 0-8014-9037-5

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.