Nenda kwa yaliyomo

Victoria Albis

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Victoria Albis (alifariki baada ya mwaka 1777) alikuwa signara kutoka Senegal. [1] Alikuwa mwakilishi maarufu wa kundi la wanawake wafanyabiashara mashuhuri waliokuwa wakijulikana kama signaras kwenye kisiwa cha Gorée huko Senegal ya Kifaransa. Alikuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa katika biashara katika Senegal ya wakati huo.

Victoria Albis alikuwa na mchanganyiko wa asili ya Kireno na Kiafrika. Alikuwa mmoja wa wakazi wa mwanzo wa jamii ya machotara waliokaa kwenye kisiwa cha Gorée baada ya Senegal kuwekwa rasmi chini ya utawala wa Ufaransa. Wao walijenga jamii hiyo katika kipindi cha kati ya 1701 hadi 1725.[2]

Jengo linalojulikana leo kama Makumbusho ya Wanawake ya Henriette-Bathily (Henriette-Bathily Women's Museum) lilijengwa na Victoria Albis.

  1. Gorée: the island and the Historical Museum. Abdoulaye Camara, Institut fondamental d'Afrique noire Cheikh Anta Diop, Joseph-Roger de Benoist, Musée historique du Sénégal.IFAN-Cheikh Anta Diop, 1993^
  2. The Business of Emotions in Modern History. (2023). Indien: Bloomsbury Publishing. p. 110
  • Gorée: the island and the Historical Museum. Abdoulaye Camara, Institut fondamental d'Afrique noire Cheikh Anta Diop, Joseph-Roger de Benoist, Musée historique du Sénégal.IFAN-Cheikh Anta Diop, 1993
  • Globalizing the Postcolony: Contesting Discourses of Gender and Development. Claire H. Griffiths. 2010