Victor Lindelof

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Victor Lindelof
Victor Lindelofakiwa na timu ya Man United.

Victor Lindelof (amezaliwa 17 Julai 1994) ni mchezaji wa timu ya taifa ya Uswidi na wa klabu ya Uingereza iitwayo Manchester United. Hucheza nafasi ya beki wa kati na pia huweza kucheza kama kiungo mkabaji.

Mchezaji huyu alisajiliwa na Manchester United kutoka Benfica huko nchini Ureno.

Lindelöf alianza kazi yake nchini Sweden katika klabu ya Västerås SK, akicheza mechi zake za kwanza Septemba 2010. Desemba 2011, alikubali kuhamia katika klabu ya Benfica nchini Ureno.

Baada ya kucheza katika timu yake ya kwanza mnamo Septemba 2013, aliendelea kuonekana katika klabu ya ngazi B, wakati pia kushinda mataji matatu ya Primeira Liga. Alijiunga na Manchester United mwezi Julai 2017.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Victor Lindelof kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.