Vanadi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Vanadi
Jina la Elementi Vanadi
Alama V
Namba atomia 23
Mfululizo safu Metali
Uzani atomia 50.9415
Valensi 2, 8, 11, 2
Densiti 6.11 g/cm³
Ugumu (Mohs) 6.7
Kiwango cha kuyeyuka 2183 K (1910 °C)
Kiwango cha kuchemka 3680 K (3407 °C)
Asilimia za ganda la dunia 0.01 %
Hali maada mango

Vanadi ni elementi na metali ya mpito yenye namba atomia 23 na alama V katika mfumo radidia wa elementi. Ni metali laini na wayaikaji yenye rangi ya kifedha-nyeupe inayotokea katika madini na kampaundi mbalimbali.

Inatumiwa kama sehemu za aloi za chumapua mbalimbali inapozuia kutu na kuongeza uwayaikaji wa chumapua. Aloi hizo zinatumiwa kwa vyombo vya kiganga kwa upasuaji, vipuri vya giaboksi, pamoja na titani katika aloi kwa matumizi ndani ya rafadha za injini za ndege.

Vanadi ina pia umuhimu fulani kwa miili ya viumbe ingawa wataalamu hawana uhakika bado vanadi inafanya kazi gani mwilini.

Picha[hariri | hariri chanzo]