Uwanja wa Wembley

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uwanja wa Wembley

Uwanja wa Wembley ni uwanja wa taifa wa mpira wa miguu huko Wembley, London, Uingereza.

Uwanja mpya ulifunguliwa mwaka 2007 mahali pa uwanja wa awali uliobomolewa mwaka 2002-2003.

Humo zinafanyika mechi kubwa za mpira wa miguu zikiwa ni pamoja na mechi za nyumbani za timu ya taifa ya Uingereza na fainali ya Kombe la FA.

Pia ni uwanja wa muda wa klabu ya soka ya Ligi Kuu ya Tottenham Hotspur huku uwanja wake White Hart Lane ukijengwa upya.

Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu zaidi kuhusu Uwanja wa Wembley kama historia yake, uenezi au kanuni zake?
Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.