Ushirika kamili

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ushirika kamili ni msamiati wa teolojia ya Ukristo kuhusu Kanisa.

Unamaanisha umoja kamili kati ya madhehebu mbalimbali kwa msingi wa imani ileile inayoyawezesha kushirikiana kikamilifu katika ibada na hasa ekaristi na sakramenti nyingine.[1]

Unatumika na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa mashariki, ukitofautishwa na ushirika usio kamili au wa kiasi tofautitofauti uliopo kati ya Wakristo wa aina zote kadiri wanavyozidi kusadiki mambo yaleyale ya msingi zaidi (kama vile Utatu mtakatifu, umungu wa Yesu Kristo na ufufuko wake), ingawa wanapishana katika mengine (hasa Kanisa na sakramenti).

Dhana ya ushirika kamili hutumiwa pia kutaja uhusiano baina ya makanisa ya Jumuiya Anglikana na pia kati ya makanisa mengine ya Kiprotestanti ambayo yameamua kutambuana na kushirikiana moja kwa moja.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. On Receiving Anglican clergy into the Catholic Church Archived 9 Februari 2001 at the Wayback Machine.; How to become a Catholic Archived 11 Juni 2009 at the Wayback Machine.; When an Orthodox joins the Catholic Church Archived 31 Agosti 2009 at the Wayback Machine.;On Participants in RCIA and Confirmation Archived 24 Septemba 2015 at the Wayback Machine.; My Return to the Catholic Church Archived 8 Mei 2007 at the Wayback Machine.; etc.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ushirika kamili kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.