Uoto asilia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Aina na wingi wa uoto wa asili.
     Tundra     Taiga     Temperate broadleaf and mixed forest     Temperate grasslands     Subtropical moist forest     Mediterranean     Monsoon forest     Jangwa     Xeric shrubland     Dry steppe     Nusu-jangwa     Grass savanna     Tree savanna     Tropical and subtropical dry forest     Tropical rainforest     Alpine tundra     Montane forest

Uoto asilia (au Uoto wa asili) ni mimea yote inayoota kiasili, tofauti na ile inayooteshwa na binadamu. Kwa hali hiyo uoto wa asili huhusiana moja kwa moja na tabia ya nchi, kwa mfano nyasi, msitu, vichaka na mbuga.

Msitu ni mkusanyiko wa miti mirefu na mikubwa ambayo huota sehemu kubwa kwa kukaribiana na vichaka ambavyo ni miti midogomidogo na mifupi iliyokusanyika kwa pamoja sana na mbuga ni uoto wa kisavana ambao ni kama nyasi.

Uoto wa asili ni matokeo ya athari za hali ya hewa, ambayo nayo huhusiana na kuathiriwa na sura ya nchi. Kwa mfano misitu minene hustawi katika sehemu za milima zenye mvua nyingi.

Aina na kiasi cha uoto wa asili hubadilika kadiri mvua inavyobadilika. WUtunzaji wa uoto wa asilia ni njia bora ya kuwezesha maisha ya afya katika jamii kwa maana kupitia njia mbalimbali za uoto wa asili kuna mvua, hewa nzuri, makazi ya wanyama. na kama utunzaji wetu wa uoto wa asilia utakuwa bora, basi utatusaidia sisi pamoja na vizazi vijavyo mbeleni.

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uoto asilia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.