Nenda kwa yaliyomo

Umakanika kawaida

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
animation of orbital velocity and centripetal acceleration
Jedwali la mwendo wa kandokando ya dunia.

Umakanika kawaida (kwa Kiingereza: classical mechanics) ni sehemu ya fizikia inayoeleza jinsi vitu vya kila siku vinavyosogea na sababu za kusogea kutokana na nguvu mbalimbali. Tukijua jinsi vitu vinavyosogea sasa, tunaweza kutabiri vitakavyosogea kesho, mbali ya kutambua vilivyosogea siku za nyuma pia. Hivyo tunaweza kutumia umakanika kawaida kuzungumzia, kwa mfano, mwendo wa sayari.

Vitu tusivyoviona, kwa mfano kutokana na udogo wake, au vinavyosogea kwa kasi mno, vinahitaji kuchunguzwa kwa umakanika kwanta ambao ni sehemu ya pili ya umakanika.

Umakanika kawaida ya kwanza ulikuwa Umakanika wa Newton, uliotengenezwa na kazi msingi wa Issac Newton na mifano ya hisabati zilivumbiliwa na Newton, Gottfried Wilhelm Leibniz, Leonhard Euler na watu wengine ili kueleza mwendo wa miili inapoathiriwa na nguvu. Baadaye njia zilizotumia nishati zilijengwa na Euler, Joseph-Louis Lagrange, William Rowan Hamilton na watu wengine ili kupeleka maendeleo ya makanika ya uchambizi (ambayo inajumuisha makanika ya Langrange na makanika ya Hamilton). Hayo maendeleo yalipanuliwa zaidi ya kazi za awali; na marekebisho fulani, yanatumika katikia maneneo yote ya fizikia ya leo[1]

  1. "Wayback Machine" (PDF). home.iitk.ac.in. Iliwekwa mnamo 2025-07-21.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Umakanika kawaida kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.