Ugonjwa wa corona Tanzania 2020

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ugonjwa wa corona uliletwa Tanzania kutoka Ubelgiji tarehe 15 Machi 2020. Msafiri aliyeleta virusi vya ugonjwa huo ni mwananchi aliyefika Arusha na ambaye baadaye alipona.

Tarehe 31 Machi 2020 Mtanzania wa kwanza alifariki huko Dar es Salaam. Waliobaki na virusi ni watu 17 kwa mujibu wa Waziri wa Afya[1].

Kufikia tarehe 19 Aprili 2020 walioambukizwa walifikia 170 na kati yao 7 wameshafariki dunia.

Dalili[hariri | hariri chanzo]

Dalili ya virusi ya corona ni

  1. Homa na mafua makali
  2. Kikohozi
  3. Kubanwa mbavu na kupumua kwa shida
  4. Mwili kuchoka
  5. Maumivu ya misuli
  6. Vidonda kooni
  7. Kuumwa kichwa

Maelekezo[hariri | hariri chanzo]

Tabia nzuri ili usipate virusi ya corona au usiambukize wengine ni

  1. Nawa mikono yako kwa maji tiririka na sabuni
  2. Funika mdomo na pua wakati wa kukohoa au kupiga chafya kwa kitambaa safi au sehemu ya mbele ya kiwiko cha mkono
  3. Kaa mbali na mtu mwenye mafua au kikohozi ambaye ana historia ya kusafiri nje ya nchi

Tabia hizo zinafanana na za Shirika la Afya Duniani

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ugonjwa wa corona Tanzania 2020 kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.