Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1884

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1884 ulikuwa wa 25 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 4 Novemba. Upande wa "Democratic Party", Grover Cleveland (pamoja na kaimu wake Thomas Hendricks) alimshinda mgombea wa "Republican Party" James Blaine (pamoja na kaimu wake John Logan).

Matokeo[hariri | hariri chanzo]

Cleveland akapata kura 219 na Blaine 182. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.