Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1856

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1856 ulikuwa wa 18 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 4 Novemba. Upande wa "Democratic Party", James Buchanan (pamoja na kaimu wake John Breckinridge) aliwashinda mgombea wa "Republican Party" John Frémont (pamoja na kaimu wake William Dayton) na mgombea wa "Know-Nothing Party", Rais wa zamani Millard Fillmore (pamoja na kaimu wake Andrew Donelson).

Matokeo[hariri | hariri chanzo]

Buchanan akapata kura 174, Frémont 114 na Fillmore nane tu. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.