Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1856
Mandhari
Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1856 ulikuwa wa 18 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 4 Novemba. Upande wa "Democratic Party", James Buchanan (pamoja na kaimu wake John Breckinridge) aliwashinda mgombea wa "Republican Party" John Frémont (pamoja na kaimu wake William Dayton) na mgombea wa "Know-Nothing Party", Rais wa zamani Millard Fillmore (pamoja na kaimu wake Andrew Donelson).
Matokeo
[hariri | hariri chanzo]Buchanan akapata kura 174, Frémont 114 na Fillmore nane tu. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya siasa bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |