Nenda kwa yaliyomo

Uainishaji wa Kimataifa wa Utendaji Kazi, Ulemavu na Afya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uainishaji wa Kimataifa wa Utendaji Kazi, Ulemavu na Afya (ICF) ni uainishaji wa vipengele vya afya vya utendaji kazi na ulemavu.

International Classification of Functioning, Disability and Health (ICF) iliidhinishwa rasmi na nchi zote 191 wanachama wa Shirika la Afya Duniani (WHO) tarehe 22 Mei 2001, wakati wa Mkutano wa 54 wa Afya Duniani.

Kupitishwa kwake kulifuatia takribani miaka tisa ya juhudi za kimataifa za kufanya marekebisho na maboresho yaliyoratibiwa na WHO.

Kabla ya ICF, WHO ilikuwa na mfumo mwingine uliojulikana kama International Classification of Impairments, Disabilities, and Handicaps (ICIDH), ambao ulianzishwa mwaka 1980 kwa ajili ya kuelezea athari za magonjwa na ulemavu kwa binadamu.[1][2]

  1. "International Classification of Functioning, Disability and Health (ICF)". World Health Organization. 22 Julai 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "International Classification of Functioning, Disability and Health (ICF)". National Center for Health Statistics. 24 Januari 2008. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 10 Mei 2009.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)