Nenda kwa yaliyomo

Tuzo za BAFTA

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kinyago cha BAFTA na nembo ya BBC ambaye amekuwa kama mtangazi wa onesho hilo tangu 1956.

Tuzo za Filamu za British Academy (kwa Kiing.: The British Academy Film Awards), zinazojulikana zaidi kama BAFTAs au Tuzo za BAFTA (BAFTA Awards), ni onyesho la kila mwaka la tuzo za filamu linaloandaliwa na British Academy of Film and Television Arts (BAFTA) ili kuheshimu michango bora ya Uingereza na kimataifa katika filamu. Hafla hiyo ilifanyika kwa mara ya kwanza katika sinema kuu ya Odeon (Odeon Cinema) iliyopo Leicester Square, London, kisha katika Royal Opera House kuanzia 2007 hadi 2016. Kuanzia 2017 hadi 2022, tukio hilo liliandaliwa katika Royal Albert Hall, kabla ya kuhamia Royal Festival Hall kwa mwaka wa 2023. Sanamu inayotolewa kwa washindi inaonyesha kinyago cha kisanii (theatrical mask).

Sherehe ya kwanza ya Tuzo za BAFTA ilifanyika mwaka 1949, na kwa mara ya kwanza ilitangazwa moja kwa moja kwenye BBC mwaka 1956, ikiwa na Vivien Leigh kama mtangazaji. Awali, sherehe hiyo ilikuwa ikifanyika mwezi Aprili au Mei; lakini tangu 2001, kwa kawaida hufanyika mwezi Februari.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu: