Tunduru

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Inapopatikana Tunduru kwenye ramani ya Tanzania

Tunduru ni mji wa Tanzania kusini na makao makuu ya wilaya ya Tunduru katika Mkoa wa Ruvuma. Umbali wake na Songea mjini ni kilomita 272; kwa usafiri wa gari unaweza kutumia muda wa saa 4-5. Jamii inayoishi Wilayani Tunduru ni Wayao, na wanategemea sana shughuli za kilimo cha korosho na sasa wamejikita sana kwenye kilimo cha mpunga. Jamii za wilaya hii inaamini sana katika masuala ya jadi yaani jando na unyago kama njia kuu ya kutolea elimu kwa vijana. Pia jamii hii inakabiliwa na tatizo kubwa la afya kutokana na uhaba wa zahanati.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Ruvuma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Tunduru kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.