Nenda kwa yaliyomo

Tshegofatso Seakgoe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Tshegofatso Seakgoe (alizaliwa Meadowlands, Gauteng, 8 Machi 1990) ni mwanamitindo na mwigizaji kutoka nchini Afrika Kusini. Mnamo mwaka 2010 alishinda shindano la uanamitindo na upigaji picha lililoendeshwa na jarida la ELLE Magazine South Africa.[1][2]

Maisha ya awali

[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa na kukulia Meadowlands, Soweto (Gauteng, Afrika Kusini) na aliishi na mama yake hadi alipofariki mwaka 1999. Baada ya hapo, alihamia kuishi na baba yake, mama wa kambo, kaka watatu wadogo, pamoja na kaka mmoja wa kambo mdogo huko Alberton, Gauteng.

Akiwa mtoto wa kike, alikuwa na nia na shauku kubwa katika tasnia ya burudani, na alishiriki katika vipindi mbalimbali vya televisheni. Miongoni mwao ni kuonekana kwenye kituo cha burudani cha watoto YOTV 4, pamoja na kuimba mbele ya Nelson Mandela katika sherehe ya kutimiza miaka 80 ya kuzaliwa. Akiwa na urefu wa futi 5 na inchi 6 (sawa na mita 1.68), mara nyingi aliamini kuwa alikuwa mfupi kupita kiasi kuweza kuwa mwanamitindo.[3]

  1. "Tshego 101". Legitimate Fashion. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2 Oktoba 2012. Iliwekwa mnamo 11 Septemba 2012.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unfit URL (link)
  2. "Local celebs reveal Christmas wish lists and plans for 2021". iol.co.za (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2021-08-11.
  3. admin. "Tshegofatso Seakgoe". Starquality (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2021-08-11.
Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tshegofatso Seakgoe kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.