Nenda kwa yaliyomo

Thoma Gaetano

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Thomas Cajetan)

Tommaso de Vio (anajulikana zaidi kama Thoma Gaetano) alikuwa mwanafalsafa na mwanateolojia wa Italia. Alihudumu kama Mkuu wa Shirika la Wahubiri kuanzia mwaka 1508 hadi 1518 na aliteuliwa kuwa kardinali mnamo 1517 hadi kifo chake.

Alikuwa mmoja wa wanateolojia mashuhuri wa wakati wake na anajulikana sana kama msemaji wa Kanisa Katoliki dhidi ya mafundisho ya Martin Luther na Matengenezo ya Kiprotestanti alipokuwa balozi wa Papa huko Augsburg. Kwa Wakatoliki, anajulikana pia kwa maoni yake ya kina kuhusu Summa Theologica ya Thoma wa Akwino.[1]

  1. Volz, J. (1908). Tommaso de Vio Gaetani Cajetan. In The Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. Retrieved September 21, 2019 from New Advent: http://www.newadvent.org/cathen/03145c.htm
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.