Theobadi wa Provins

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake huko Joigny.

Theobadi wa Provins, O.S.B. Cam. (kwa Kifaransa: Thibaud; 103330 Juni 1066) alikuwa mtoto wa mtawala wa Champagne, Ufaransa[1], aliyevutiwa sana na maisha ya Yohane Mbatizaji na ya Mababu wa jangwani[2], hivyo akaenda kujiunga na monasteri huko Reims.

Baadaye, akiongozana na rafiki Walter, aliishi kama mkaapweke katika mahali na nchi mbalimbali ili kukwepa watu waliowatafuta ili kuwaheshimu[3].

Kabla hajafa alipewa upadrisho ili kuongoza vizuri zaidi wanafunzi alioanza kupokea akajiunga na Wabenedikto Wakamaldoli huko Sassano, Italia[4].

Papa Aleksanda II alimtangaza mtakatifu mwaka 1073.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Juni[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. François Verdier, Saints de Provins et comtes de Champagne. Essai sur l'imaginaire médiéval, Guéniot, Langres 2007.
  2. H. Pomeroy Brewster, Saints and festivals of the Christian Church, F.A. Stokes, 1904, pp. 314-315.
  3. Löffler, Klemens. "St. Theobald." The Catholic Encyclopedia Vol. 14. New York: Robert Appleton Company, 1912. 1 August 2017
  4. http://www.santiebeati.it/dettaglio/92850
  5. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.