Teofilo wa Antiokia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Teofilo wa Antiokia (kwa Kigiriki Θεόφιλος ὁ Ἀντιοχεύς, Theofilos o Antiokheus, alifariki 183/185 BK) alikuwa Patriarki wa Antiokia[1] baada ya Eros na kabla ya Maximus I[2][3].

Kutoka maandishi yake (Eusebi wa Kaisarea na Jeromu walitaja vitabu mbalimbali vya Teofilo vilivyokuwepo nyakati zao, ambavyo kati yake kimebaki kile Utetezi kwa Autolycus[4], rafiki yake msomi lakini Mpagani) tunajua kwamba alizaliwa na Wapagani katika eneo la mito Tigri na Eufrate, na kwamba aliingia Ukristo kwa kusoma Biblia, hasa vitabu vya kinabii.[5]

Kutoka kwa mwanahistoria Eusebius wa Kaisarea tunajua juhudi zake za kupinga uzushi, hasa ule wa Marcion[6], akichangia fasihi ya Kikristo, hoja za dini, ufafanuzi wa Biblia na utetezi wa dini.[7]

Maandishi yake ndiyo ya zamani kuliko yale yote tuliyonayo yanayotaja Utatu Mtakatifu.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 13 Oktoba[8].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Eusebius, Ecclesiastical History iv. 20; Jerome Ep. ad Algas. quaest. 6.
  2. Henry Fynes Clinton, Fasti Romani
  3. John Lightfoot, S. Ignatius, vol. ii. p. 166.
  4. Jacques Paul Migne's Patrologia Graeca, t. vi. col. 1023-1168 and a small edition (Cambridge 1852) by W. G. Humphry. Johann Carl Theodor von Otto's edition in the Corpus apologetarum christianorum saeculi secundi vol. ii. (Jena, 1861) is by far the most complete and useful. English translations by Joseph Betty (Oxford 1722), W. B. Flower (London, 1860), Marcus Dods (Clark's Ante-Nicene Library), and Robert M. Grant (Clarendon Press, 1970).
  5. Apologia ad Autolycum i. 14, ii. 24.
  6. Ecclesiastical History iv. 24.
  7. William Sanday, Studia Biblica, p. 90 describes him as "one of the precursors of that group of writers who, from Irenaeus to Cyprian, not only break the obscurity which rests on the earliest history of the Church, but alike in the East and in the West carry it to the front in literary eminence, and distance all their heathen contemporaries".
  8. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.