Tausi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tausi
Tausi wa Kongo
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Galliformes (Ndege kama kuku)
Familia: Phasianidae (Ndege walio na mnasaba na kwale)
Jenasi: Afropavo Chapin, 1936

Pavo Linnaeus, 1758

Tausi ni ndege wakubwa wa jenasi Pavo na Afropavo katika familia ya Phasianidae.

Dume ana rangi ing’aayo ya majani au buluu na mkia wake ni mrefu mwenye rangi nyingi. Jike ana rangi inayofifia pengine kahawia tu. Jinsia zote zina ushungi. Dume hukoga mkia kwa ubembelezi.

Hula matunda, maua, wadudu na watambazi. Hutaga mayai matatu hadi manane ardhini.

Tausi wa Kongo anatokea Kongo ya Kidemokrasia. Spishi mbili nyingine zinatokea misitu ya Asia, lakini zimewasilishwa katika sehemu nyingine za dunia, hususa tausi mhindi.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za Asia[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]