Nenda kwa yaliyomo

Tabitha Siwale

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Tabitha Siwale (Tukuyu, 28 Julai 1938 - Dar es Salaam, 12 Machi 2025) alikuwa Mtanzania mwanamke wa kwanza kupata kuwa waziri wa nchi mwaka 1975.[1]

Tabitha Ijumba Wilfred Mwambenja alizaliwa mwaka 1938 Tukuyu, eneo lililokuwa linajulikana wakati huo kama Tanganyika Territory.[2][3] Baba yake, Wilfred Mwambenja, pamoja na ndugu wengine wa familia yao, walihusika katika harakati za kisiasa wakati wa mapambano ya uhuru wa nchi.[2]

Baada ya kusoma katika shule ya msingi ya Native Authority, mwaka 1951 alijiunga na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Tosamaganga.[2][3]

Baada ya kuendelea na masomo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Geita na Chuo cha Ualimu cha Mpwapwa, Siwale alianza kazi ya ualimu mwaka 1961.[2][3] Kati ya mwaka 1965 na 1968, alisoma home economics katika Chuo Kikuu cha Nairobi.[2][3] Aliporejea Tanzania, aliendelea na taaluma ya ualimu na hatimaye alipandishwa cheo na kuwa mwalimu mkuu katika shule kadhaa.[2][3]

Siwale na mumewe walibarikiwa kupata watoto wanne: Fred, Mary, Abel, na Maka.[2] Mume wake alifariki dunia mwaka 2016.[2] Tabitha Siwale alifariki dunia mwaka 2025 akiwa na umri wa miaka 86 katika jiji la Dar es Salaam.[2][4][5]

  1. https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/usichofahamu-kuhusu-waziri-wa-kwanza-mwanamke-tanzania-4964370
  2. 1 2 3 4 5 6 7 8 9 wa Atikali, Mzee (2025-03-14). "Usichofahamu kuhusu waziri wa kwanza mwanamke Tanzania". Mwananchi. Iliwekwa mnamo 2025-03-26.
  3. 1 2 3 4 5 Africa Woman (kwa Kiingereza). Africa Journal Limited. 1975.
  4. "Former Minister Tabitha Siwale passes away". Daily News (kwa American English). 2025-03-13. Iliwekwa mnamo 2025-03-26.
  5. "Waziri wa kwanza mwanamke Tanzania afariki dunia". Mwananchi. 2025-03-13. Iliwekwa mnamo 2025-03-26.
Makala hii kuhusu kuhusu mwanasiasa wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tabitha Siwale kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.