Susan Kihika
Mandhari
| Susan Kihika | |
|---|---|
| Amezaliwa | Susan Wakarura Kihika |
| Uraia | Mtu wa kenya |
| Kazi yake | Mwanasheria,mwanasiasa |
| Chama cha siasa | Jubilee Party |
| Ndoa | Mume na Watoto wawili |
Susan Wakarura Kihika ni mwanasheria na mwanasiasa wa Kenya, na gavana wa kwanza mwanamke wa Kaunti ya Nakuru. Pia alikuwa miongoni mwa magavana saba wanawake waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu wa Kenya wa tarehe 9 Agosti 2022, kati ya jumla ya magavana 40 wanaume. Hili lilionyesha maendeleo makubwa ikilinganishwa na magavana wanawake watatu pekee waliochaguliwa katika uchaguzi wa mwaka 2017.
Historia na Elimu
[hariri | hariri chanzo]Alice, mama yake, alikuwa mke wa pili wa baba yake[1]. Susan alisoma katika Busara Forest View Academy huko Nyahururu na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Bishop Gatimu Ngandu huko Nyeri.[2] Baadaye, mnamo takribani mwaka 1992, alihamia Marekani kwa ajili ya kuendelea na masomo yake.[3]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mwanasiasa huyo wa Kenya bado ni mbegu. Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |