Nenda kwa yaliyomo

Susan Kihika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Susan Kihika
AmezaliwaSusan Wakarura Kihika 
UraiaMtu wa kenya
Kazi yakeMwanasheria,mwanasiasa
Chama cha siasaJubilee Party
NdoaMume na Watoto wawili

Susan Wakarura Kihika ni mwanasheria na mwanasiasa wa Kenya, na gavana wa kwanza mwanamke wa Kaunti ya Nakuru. Pia alikuwa miongoni mwa magavana saba wanawake waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu wa Kenya wa tarehe 9 Agosti 2022, kati ya jumla ya magavana 40 wanaume. Hili lilionyesha maendeleo makubwa ikilinganishwa na magavana wanawake watatu pekee waliochaguliwa katika uchaguzi wa mwaka 2017.

Historia na Elimu

[hariri | hariri chanzo]

Alice, mama yake, alikuwa mke wa pili wa baba yake[1]. Susan alisoma katika Busara Forest View Academy huko Nyahururu na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Bishop Gatimu Ngandu huko Nyeri.[2] Baadaye, mnamo takribani mwaka 1992, alihamia Marekani kwa ajili ya kuendelea na masomo yake.[3]